Saturday 12 August 2017

USHIRIKI WA UJANA NI MTAJI PROGRAM KATIKA MAONESHO YA 25 NANENANE MOROGORO

Mchoraji akiwa kazini akiandika kilichokua kinatarajiwa kufannywa na timu ya Ujana ni Mtaji.
Timu ya Ujana ni Mtaji iliyochini ya taasisi ya Faraja Trust Fund ikishirikiana na taasisi ya vijana inayojulikana kama Lights Up Youth Foundation ilishiriki maonesho ya 25 ya nanenane yaliyofanyika katika viwanja vya Mwl. Nyerere Morogoro yaliyokua na kauli mbiu  ZALISHA KWA TIJA MAZAO NA BIDHAA ZA KILIMO ,MFUGO NA UVUVI ILI KUFIKA UCHUMI WA KATI".kuanzia agosti 1-10.

Katika maonesho hayo Ujana ni Mtaji ilifanya baadhi ya shughuli ambazo ni Kutoa elimu ya lishe, Kupima uwiano wa mwili (BMI), Msaada wa kisheria, Elimu ya ujasiriamali pamoja na kutoa ushauri nasaha na kupima virusi vya ukimwi (VVU) kwa hiari. Ushiriki huu wa Ujana ni Mtaji ni kwa mara ya kwanza lengo likiwa kuwafikia watanzania wengi zaidi hasa wenye uhitaji wakiwemo wakulima.
Wanafunzi kutoka shule ya wasichana Ifakara wakipata maelezo mbalimbali kutoka kwa timu ya Ujana ni Mtaji.
Tulitembelewa na watu kutoka makundi tofauti kutoka katika jamii zetu wakiwemo watoto, wafugaji, wakulima wa kawaida, watu wa makundi maalumu, viongozi wa dini na viongozi wa serikali. Idadi ya waliotembelea banda letu ilikua kubwa na tunashukuru kwa wote waliojitokeza na kupata huduma kutoka kwa timu ya Ujana ni Mtaji.
Mtoto akipimwa uzito wakati wa maonesho ya 25 nanenane viwanja vya Mwl Nyerere, Morogoro.
Mfugaji jamii ya masai akipewa ushauri kuhusiana na masuala ya lishe baada ya kupima uwiano wa mwili 



Wachekeshaji walipita pia katika banda la Ujana ni Mtaji kupata elimu






Pia katika maonesho hayo banda la Ujana ni Mtaji lilitembelewa na Meya wa Manispaa ya Morogoro mjini Mh. Pascal Kihanga ambaye alielezwa kuhusiana na program kwa ufupi na alishiriki katika vipimo vya uwiano wa mwili pamoja na kupata elimu ya lishe bila kusahau alimalizia sehemu iliyohusu elimu ya ujasiriamali na msaada wa kisheria.
Mh. Pascal Kihanga ambaye ni Meya wa manispaa ya Morogoro akielezwa kwa ufupi kuhusiana na programu





Ndugu Yahya Naniya (kulia) kutoka ofisi ya mkuu wa wilaya Morogoro ambaye ndiye alikua mwenyeji wa Meya akisikiliza jambo kwa makini.
Ujana ni Mtaji inaamini kwenye nguvu na mchango wa wanawake katika maendeleo hasa kuelekea uchumi wa kati na kwa bahati njema tulitembelewa na mke wa mkuu wa mkoa wa Morogoro Mama Leonia Kebwe ambapo alihudumiwa vizuri na timu ya vijana ya Ujana ni Mtaji programu na furaha aliyoondoka nayo kwetu ni baraka tosha.


Kwa njia ya pekee tunatambua mwitikio na shauku ya wananchi katika kujua afya zao, sio upande wa uwiano wa mwili bali hadi kwenye kupima maambukizi ya virusi vya ukimwi (VVU) bila kusahau ushauri nasaha.
Sehemu mahsusi iliyokua inatumika kwa ajili ya ushauri nasaha pamoja na kupima virusi vya ukimwi (VVU) kwa hiari



Pia Uongozi wa taasisi shiriki unatoa shukrani za dhati kwa wote waliojitokeza kwa njia moja au nyengine kuwakaribisha watu katika banda letu la Ujana ni Mtaji wakati wote wa maonesho.

Ujana ni Mtaji programu bado ipo kwenye mchakato wa ufunguzi ambao unatarajiwa kufanyika mda sio mrefu ambapo unaratibiwa na kamati maalumu inayoundwa kwa kushirikiana kwa taasisi za FARAJA TRUST FUND na LIGHTS UP YOUTH FOUNDATION pamoja na wadau mbalimbali wa maendeleo kwa kushirikiana na ofisi ya mkurugenzi, mkuu wa wilaya na mkuu wa mkoa Morogoro.
Kamati ya maandalizi ya programu ya Ujana ni Mtaji iliyokutana tarehe 25 mwezi wa tano mwaka huu katika ofisi za Faraja Trust Fund.







SHARE THIS

Author:

Facebook Comment

0 comments: